Barua taka

Maelezo ya sera

BADILISHA KUMBUKUMBU
Utaratibu wa Sera
Haturuhusu maudhui ambayo yameundwa ili kudanganya, kupotosha au kuwalemea watumiaji ili kuongeza utazamaji kibandia. Maudhui haya huzuia uwezo wa watu kuingiliana kihalali katika majukwaa yetu na kutishia usalama, imara, na uwezo wa kutumika kwa huduma zetu. Pia tunajitahidi kuzuia mbinu za matumizi mabaya, kama vile kueneza viungo vya kudanganya ili kuwavutia watumiaji ambao hawashuku kupitia utendaji au msimbo wa kupotosha au kuiga kikoa kinachoaminika.
Barua taka za mtandaoni ni tasnia ya faida kubwa. Sera na ugunduzi wetu lazima zibadilike kila mara ili kuendana na mitindo na mbinu zinazoibuka za barua taka. Katika kuchukua hatua ya kukabiliana na barua taka, tunataka kusawazisha kuongeza gharama kwa watayarishaji na wasambazaji wake kwenye mifumo yetu, kwa kulinda shughuli mahiri na halisi ya jumuiya yetu.
Haturuhusu:
  • Kuchapisha, kushiriki, kujihusisha na maudhui au kufungua akaunti, Vikundi, Kurasa, Matukio au rasilimali nyingine, ama kikuli au kiotomatiki mara nyingi zaidi.
    • Tunaweza kuweka vizuizi dhidi ya akaunti ambazo zinatumika mara chache wakati viashiria vingine vya Taka (k.m., uchapishaji wa maudhui yanayojirudia) au ishara za kutokuwa halali zipo.
  • Kujaribu au kufaulu kuuza, kununua au kubadilisha rasilimali za jukwaa, kama vile akaunti, vikundi, kurasa, n.k.
  • Kujaribu au kufaulu kuuza, kununua, au kubadilisha idhini za tovuti, kama vile majukumu ya msimamizi au mratibu, au kibali cha kuchapisha kwenye sehemu mahususi.
  • Kujaribu au kufaulu kuuza, kununua, au kubadilisha maudhui ili kupata kitu chenye thamani ya pesa, isipokuwa Maudhui yenye Chapa yaliyotambuliwa kwa wazi, kama ilivyofafanuliwa kwenye Sera za Maudhui yenye Chapa.
  • Kujaribu au kufaulu kuuza, kununua au kubadilisha ili kupata uhusiano, kama vile, vipendwa, kushiriki, mionekano, ufuasi, mibofyo, matumizi ya alama mahususi za reli, n.k. Haya ni pamoja na:
    • Kutoa tunu (yaani., kuwapa watu wengine fursa ya kushinda) pesa taslimu au zawadi zenye thamani sawa na pesa ili kupata uhusiano. (k.m., “Mtu yeyote atakayependa ukurasa wangu atajiunga ili kushinda $500”)
    • Kuahidi kutoa chochote chenye thamani ya pesa ili kupata uhusiano. (k.m., “ukipenda ukurasa wangu, nitakupa iPhone!”)
  • Kutaka au kudai kuwa watumiaji wanahitajika kujihusisha na maudhui (k.m., kupenda, kushiriki) kabla ya kuweza kutazama au kuingiliana na maudhui waliyoahidiwa.
  • Kushiriki URL, vikoa au programu za udanganyifu au za kupotosha ikiwa ni pamoja na:
    • Unyemelezi: Unyemelezi ni jaribio lolote la kuepuka sera zetu za maudhui kwa kuwasilisha kimakusudi maudhui tofauti ya nje ya jukwaa, kama vile URL au programu, kwenye mifumo yetu ya uadilifu ikilinganishwa na kinachoonyeshwa kwa watumiaji.
    • Viungo vya Kupotosha: Maudhui yaliyo na kiungo kinachoahidi aina moja ya maudhui lakini kinawasilisha kitu ambacho kina maudhui tofauti. Hii inaweza kujumuisha maudhui yaliyo kwenye programu iliyoahidiwa.
    • Tabia ya kuelekeza kwingine kwa udanganyifu: Tovuti zinazohitaji kitendo (k.m, captcha, tazama tangazo, bofya hapa) ili kutazama maudhui tarajiwa kwenye ukurasa wa kutua na jina la kikoa la URL kubadilika baada ya kitendo kinachohitajika kukamilika, au kuelekeza watumiaji kiotomatiki kwenye kikoa tofauti kabisa bila mtumiaji kufanya kitendo chochote.
    • Kuruhusiwa kufikia maudhui baada ya kupenda/kushiriki: Kuwataka watumiaji kujihusisha (kwa njia ya vipendwa, kushiriki, ufuasi au aina nyingine yoyote ya uhusiano unaopatikana kwa umma) ili kupata uwezo wa kufikia maudhui mahususi ya kipekee.
    • Utendakazi wa udanganyifu wa jukwaa - Kuiga vipengele au utendakazi wa huduma zetu, kama vile kuiga uchangishaji, kura za maoni za ndani, vitufe vya kucheza, au kitufe cha Kupenda ambapo utendakazi huo haupo au haufanyi kazi inavyotarajiwa, ili kumfanya mtumiaji afuate kiungo.
    • Utendakazi danganyifu wa ukurasa wa kutua: Tovuti zilizo na violesura vya watumiaji vya kupotosha, ambavyo vinasababisha trafiki kuzalishwa kimakosa (k.m. madirisha ibukizi ya juu/chini, kuhadaa watu kwa kuwafanya kubofya viungo, n.k). Hii ni pamoja na mbinu kama vile kutumia mitego, ambapo madirisha ibukizi yasiyo muhimu yanajitokeza mtu anapojaribu kuondoka kwenye ukurasa wa kutua.
    • Kuiga Ukurasa wa kutua au kikoa - Ukurasa wa kutua wa nje ya jukwaa, URL au tovuti au kikoa cha nje kinachojifanya kuwa chapa au huduma yenye hadhi kwa kutumia jina, kikoa au maudhui ambayo yanaangazia makosa ya hijai, tahajia au njia nyingine za kuiga tovuti, vikoa au chapa maarufu, kwa kutumia ukurasa wa kutua unaofanana na wa tovuti zinazoaminika.
    • Matumizi mengine ya udanganyifu ya URL au viungo ambayo yanafanana sana na yaliyo hapo juu.
  • Licha ya yaliyo hapo juu, hatujapiga marufuku:
    • Tangazo la majukwaa anuwai ambalo halijachochewa na malipo kwa mhusika mwingine
    • Kuhamisha wajibu wa msimamizi na mratibu wa ukurasa au kikundi kwa mtumiaji mwingine kulingana na mambo yanayomvutia kwenye ukurasa au kikundi hicho, badala ya kubadilishana thamani.
    • Kuchapisha au kushiriki Maudhui yenye Chapa yaliyotambuliwa wazi.
Hali ya matumizi ya mtumiaji
Tazama mifano kadhaa ya jinsi utekelezaji unavyoonekana kwa watu kwenye Facebook, kama vile: inavyoonekana kuripoti kitu ambacho unafikiri hakipaswi kuwa kwenye Facebook, kuambiwa kuwa umekiuka Viwango vyetu vya Jumuiya na kuona skrini ya onyo juu ya maudhui fulani.
Dokezo: Tunaendelea kuboresha, kwa hivyo kile unachokiona hapa kinaweza kupitwa na wakati kiasi ikilinganishwa na kile tunachotumia sasa.
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Kuripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Mawasiliano ya baada ya ripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Hali ya kuondoa
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Skrini za onyo
Data
Tazama Ripoti ya sasa ya Utekelezwaji wa Viwango vya Jumuiya
Utekelezaji
Tuna sera sawa ulimwenguni kote, kwa ajili ya kila mtu kwenye Facebook.
Timu za ukaguzi
Timu yetu ya kimataifa ya wakaguzi zaidi ya 15,000 hufanya kazi kila siku kuweka watu kwenye Facebook kuwa salama.
Ushiriki wa mshikadau
Wataalamu wa nje, wasomi, mashirika yasiyo ya faida na watungaji sera husaidia kuweka Viwango vya Jumuiya ya Facebook.
Pata usaidizi wa baruataka
Jifunze unachoweza kufanya ukiona kitu kwenye Facebook ambacho kinakiuka Viwango vyetu vya Jumuiya.
Tembelea Kituo chetu cha Usaidizi