Uombaji wa Ngono kutoka kwa Watu Wazima na Lugha Chafu ya Kingono

Maelezo ya sera

BADILISHA KUMBUKUMBU
Utaratibu wa Sera
Kama ilivyodokezwa katika sera ya Unyanyasaji wa Watu Wazima Kingono, watu hutumia huduma zetu kujadili na kuangazia vurugu na unyanyasaji kingono. Tunatambua umuhimu wa na tunaruhusu mjadala huu uendelee. Pia tunaruhusu mjadala kuhusu utetezi wa haki za wafanyakazi wa ngono na udhibiti kwa kazi za kingono. Hata hivyo, tunaweka mipaka, wakati maudhui yanawezesha shughuli za kingono au huduma za biashara ya ngono kati ya watu wazima au wakati maudhui yanaomba au kutoa maudhui ya ponografia au maudhui ya kingono. Tunafanya hivyo ili kuzuia uwezeshaji wa miamala inayoweza kujumuisha ulanguzi, kutumia nguvu na vitendo vya ngono bila idhini.
Pia tunawekea mipaka lugha dhahiri ya kingono ambayo inaweza kusababisha uombaji wa ngono kwa sababu baadhi ya hadhira ndani ya jumuiya yetu kote ulimwenguni wanaweza kuathirika sana na aina hii ya maudhui na inaweza kuzuia uwezo wa watu kuunganishwa na marafiki zao na jumuiya pana zaidi.
Haturuhusu:
Maudhui yanayotoa, kuuliza au kutoa mbinu za mawasiliano ya ukahaba, ambayo inafafanuliwa kuwa kuomba au kujitolea kwa ajili ya shughuli za ngono ili kupata pesa au chochote chenye thamani kwa:
  • Kutoa au kuuliza shughuli za ngono (kwa mfano, huduma za ngono, uchuaji wa misuli wenye asili ya ngono/kuchochea ngono, gumzo/mazungumzo ya ngono, huduma za utawala)
  • Kutumia maneno ya misimu ya kurejelea ukahaba pamoja na kuomba au ofa ya upatikanaji, bei au ishara yoyote ya muamala wa pesa au kitu chenye thamani, eneo au maelezo ya mwasiliani
  • Kushiriki katika uombaji wa ngono pamoja na bei au ishara yoyote ya muamala wa pesa au kitu chenye thamani
  • Kuonyesha au kutaja shughuli au washirika wa ngono na bei au ishara zozote za kifedha au miamala ya ukarimu.
  • Kuajiri au kutoa ofa kwa watu wengine ili kupata kazi ya biashara ya ngono kunashughulikiwa na sera dhidi ya Unyanyasaji wa Binadamu.
Maudhui yanayoshiriki katika uombaji wa ngono kwa, kutoa, kuomba au kuonyesha mbinu za mawasiliano ya shughuli za ngono kama vile:
  • Tendo la ngono au uamshaji wa ngono
  • Ngono ya kinywani
  • Mienendo isiyo ya kawaida ya ngono
  • Magumzo au mazungumzo ya ngono
  • Ujumbe wa kingono au chafu
  • Dansi za kingono au kuvua nguo
  • Kutuma taswira za uchi (kama vile picha za uchi, video za ngono)
Maudhui yanayoomba, kutoa au kuonyesha mbinu za mawasiliano ili kupata nyenzo za ponografia au zilizo na majina ya mtumiaji au viungo vya kujiunga na tovuti za ponografia.
Lugha chafu ya kingono inayotumia maelezo ya wazi au ya kuogofya kuhusu:
  • Viungo vya uzazi,
  • Hali za kupata ashiki ya ngono (k.m., kutoa manii au dhakari kupata joto)
  • Matukio ya Ngono
  • Yaliyo hapa juu hayajumuishi maudhui yaliyoshirikiwa katika muktadha wa ucheshi, tashtiti au kukemea tendo la ngono
Tunaruhusu maudhui ambayo yanashughulikiwa vinginevyo na sera hii yanapochapishwa katika miktadha ya kulaani, kuelimisha, kuongeza uhamasishaji au kuripoti habari. Pia hatupigi marufuku majadiliano kuhusu vitendo vya kingono chini ya sera hii. Hata hivyo, huenda haya yakaruhusiwa tu kwa watu wazima wenye umri wa zaidi ya miaka 18 kulingana na sera ya Afya na Ustawi ili kuwezesha hali za utumiaji zinazofaa kiumri kwa watoto.
Kwa maudhui yafuatayo, tunazuia uwezo wa kutazama maudhui kwa watu wazima, wa umri wa miaka 18 na zaidi:
  • Maudhui yanayojadili tabia au hali za kingono
  • Maudhui ambayo yana majina ya watumiaji, viungo au nembo za Tovuti za Usajili wa Watu Wazima
  • Lugha chafu ya kingono katika miktadha ya ucheshi au tashtiti, ikiwa ni pamoja na sitiari za kingono
  • Lugha inayoashiria ngono ambayo inarejelea shughuli za kingono
Kwa Viwango vya Jumuiya vifuatavyo, tunahitaji maelezo ya ziada na/au muktadha ili kutekeleza:
  • Katika kesi fulani, tutaruhusu maudhui ambayo vinginevyo yanaweza kukiuka Viwango vya Jumuiya inapobainika kwamba maudhui hayo ni ya tashtiti. Maudhui yataruhusiwa tu ikiwa vipengee vinavyokiuka vya maudhui hayo vimefanywa kama vya tashtiti au kuhusishwa na kitu au mtu ili kumdhihaki au kumsuta.
Hali ya matumizi ya mtumiaji
Tazama mifano kadhaa ya jinsi utekelezaji unavyoonekana kwa watu kwenye Facebook, kama vile: inavyoonekana kuripoti kitu ambacho unafikiri hakipaswi kuwa kwenye Facebook, kuambiwa kuwa umekiuka Viwango vyetu vya Jumuiya na kuona skrini ya onyo juu ya maudhui fulani.
Dokezo: Tunaendelea kuboresha, kwa hivyo kile unachokiona hapa kinaweza kupitwa na wakati kiasi ikilinganishwa na kile tunachotumia sasa.
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Kuripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Mawasiliano ya baada ya ripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Hali ya kuondoa
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Skrini za onyo
Utekelezaji
Tuna sera sawa ulimwenguni kote, kwa ajili ya kila mtu kwenye Facebook.
Timu za ukaguzi
Timu yetu ya kimataifa ya wakaguzi zaidi ya 15,000 hufanya kazi kila siku kuweka watu kwenye Facebook kuwa salama.
Ushiriki wa mshikadau
Wataalamu wa nje, wasomi, mashirika yasiyo ya faida na watungaji sera husaidia kuweka Viwango vya Jumuiya ya Facebook.
Pata usaidizi kuhusiana na uombaji wa ngono kutoka kwa mtu mzima na lugha chafu ya kingono.
Jifunze unachoweza kufanya ukiona kitu kwenye Facebook ambacho kinakiuka Viwango vyetu vya Jumuiya.
Tembelea Kituo chetu cha Usaidizi