Tabia ya Chuki

Maelezo ya sera

BADILISHA KUMBUKUMBU
Utaratibu wa Sera
Tunaamini kwamba watu hutumia sauti zao na kuunganika kwa urahisi zaidi wakati hawahisi kushambuliwa kwa msingi wa wao ni akina nani. Hiyo ndio maana haturuhusu tabia ya chuki kwenye Facebook, Instagram, au Threads.
Tunafafanua tabia ya chuki kama mashambulio ya moja kwa moja dhidi ya watu — badala ya dhana au taasisi — kulingana na kile tunachoweza kukiita kama sifa zinazolindwa (PCs): rangi, kabila, asili ya kitaifa, ulemavu, mrengo wa kidini, tabaka, mwelekeo wa kingono, jinsia, utambulisho wa kijinsia, na ugonjwa hatari. Zaidi ya hayo, tunazingatia umri kuwa sifa inayolindwa inaporejelewa pamoja na sifa nyingine inayolindwa. Pia tunawalinda wakimbizi, wahamiaji wa muda, wahamiaji wa kudumu, na wanaotorokea usalama wao kutokana na mashambulizi makali zaidi (Kiwango cha 1 hapa chini), ijapokuwa tunaruhusu maoni kuhusu na ukosoaji wa sera za uhamiaji. Vivyo hivyo, tunatoa baadhi ya ulinzi kwa sifa zisizolindwa, kama vile kazi, zinaporejelewa pamoja na sifa iliyolindwa. Wakati mwingine, kulingana na matumizi ya kindani, tunazingatia baadhi ya maneno au virai kama viwakilishi vinavyotumika mara kwa mara kwa sifa zilizolindwa.
Tunaondoa kauli za kudhalilisha, tuhuma za hali mbaya ya ukosefu wa maadili au uhalifu na maneno ya ubaguzi. Pia tunaondoa kasumba mbaya, ambayo tunafafanua kama ulinganishaji usio na utu ambazo kihistoria zimekuwa zikitumika kushambulia, kutisha, au kutenga vikundi mahususi, na ambayo mara nyingi huhusishwa na vurugu vya nje ya mtandao. Hatimaye, tunaondoa matusi mabaya, hali za kuonyesha madharau au kughafilika, kulaani na miito ya kutengwa au ubaguzi watu wanapolengwa kulingana na sifa zilizolindwa. Tunagawa kauli hii kwenye safu mbili za uzito, kama ilivyofafanuliwa hapa chini.
Tunatambua kwamba wakati mwingine watu wanashiriki maudhui ambayo yanajumuisha ubaguzi na matamshi ya chuki ya mtu mwingine ili kukashifu matamshi hayo au kuyaripoti. Katika visa vingine, matamshi ya chuki, ikiwemo ubaguzi, ambayo yanaweza vinginevyo kukiuka viwango vyetu hutumika katika urejeleaji binafsi au kwa namna ya kutia nguvu. Tunaruhusu aina hii ya matamshi ambapo nia ya mzungumzaji ni wazi: Wakati kusudi la kushiriki halibainishwi, tunaweza kuondoa maudhui.
Wakati mwingine watu hutumia lugha inayobagua wengine kulingana na ngono au jinsia wanapojadili ufikiaji wa nafasi ambazo mara nyingi huwa na mipaka ya ngono au jinsia, kama vile ufikiaji wa vyoo, shule mahususi, jeshi mahususi, utekelezaji wa sheria au nafasi za ufundishaji na vikundi vya afya au usaidizi. Wakati mwingine, zinatoa mwito wa kubaguliwa au kutumia lugha ya matusi katika muktadha wa kujadili mada za kisiasa au kidini, kama vile wanapojadili haki za watu wanaobadilisha jinsia zao, wahamiaji au wenye mahusiano ya jinsia moja. Hatimaye, wakati mwingine watu hulaani jinsia fulani katika muktadha wa kuvunja uhusiano wa kimapenzi. Sera zetu zimeundwa ili kutoa nafasi ya aina hizi za matamshi.
Usichapishe:
Ngazi ya 1
Maudhui yanayolenga mtu au kikundi cha watu (isipokuwa vikundi vilivyoelezwa kuwa vimewahi kufanya uhalifu au vurugu za kingono au kuwakilisha takriban nusu ya kikundi) kwa msingi wa sifa zao zinazolindwa ambazo zimetajwa au hali ya uhamiaji katika namna ya maandishi au picha na:
  • Matamshi ya kudhalilisha kwa namna ya ulinganishaji au utoaji kauli za jumla kuhusu wanyama, viini vya magonjwa au namna nyingine za maisha ya mwanadamu, ikiwa ni pamoja na:
    • Wadudu (pamoja na lakini si tu kwa: mende, nzige)
    • Wanyama kwa ujumla au aina mahususi za wanyama wanaochukuliwa kitamaduni kuwa duni (ikiwemo lakini sio tu kwa: Watu weusi na wanyama jamii ya sokwe au viumbe vinavyofanana na sokwe; Watu wayahudi na panya; Watu waislamu na nguruwe; Watu wa Mexico na minyoo)
    • Bakteria, virusi au vijidudu
    • Binadamu mwenye upungufu (ikiwemo lakini sio tu kwa: washenzi, mashetani, mizuka)
  • Tuhuma za hali mbaya ya ukosefu wa maadili na uhalifu:
    • Washambuliaji wa kingono na wanaonajisi watoto (ikijumuisha lakini si tu kwa: Waislamu wanaofanya ngono na mbuzi au nguruwe)
    • Wahalifu wa vurugu (ikiwemo lakini si tu kwa: magaidi, wauaji)
  • Miito na matumaini ya madhara yafuatayo (matishio mabaya au mahususi na miito ya vurugu hushughulikiwa chini ya sera yetu ya Vurugu na Uchochezi):
    • Kuambukizwa ugonjwa
    • Kupitia hali ya maafa asili
    • Kujijeruhi au kujitoa uhai
    • Kifo bila mhalifu au mbinu
    • Ajali na madhara mengine ya kimwili yanayosababishwa na mhalifu au na Mungu
  • Kasumba mbaya ambazo kihistoria zinaunganishwa na vitisho au vurugu, kama vile Blackface; Kukataliwa kwa uangamizaji wa kabila; madai kwamba Wayahudi wanadhibiti taasisi za fedha, kisiasa, au vyombo vya habari; na marejeo ya Dalits kama wafanyakazi wa hali ya chini; na kulinganisha watu Weusi na vyombo vya shambani.
  • Kukejeli dhana, matukio au waathirika wa uhalifu wa chuki hata iwapo hakuna mtu halisi aliyetambulika kwenye picha.
  • Kudhihaki watu kwa kuwa wana ugonjwa au wanapitia hali ya ugonjwa.
  • Maudhui yanayoeleza au kuwalenga watu kwa njia hasi kupitia maneno ya ubaguzi. Maneno ya ubaguzi yanafafanuliwa kama maneno ambayo kiasili yanaunda mazingira ya kutenga na vitisho dhidi ya watu kwa msingi wa sifa iliyolindwa, mara nyingi ni kwa sababu maneno haya yanahusishwa na ubaguzi, udhalimu, na uhasama wa kihistoria.
Ngazi ya 2
Maudhui yanayolenga mtu au kikundi cha watu kwa msingi wa sifa zao zinazolindwa (katika muundo wa maandishi wa kutazama) na:
  • Wito au usaidizi wa kutengwa au kubagua au kauli za nia ya kutenga au kubagua, kama ilivyofafanuliwa:
    • Ubaguzi wa jumla, ambayo inamaanisha kutoa mwito wa kutenga au kubagua kwa jumla, kama vile “Hakuna X inayoruhusiwa!”
    • Ubaguzi wa kisiasa, ambayo inamaanisha kukataa haki ya kushiriki katika siasa au kutoa mwito wa kufungwa au kunyima haki za kisiasa.
    • Kutengwa kiuchumi, ambayo inamaanisha kunyimwa haki ya kufikia haki za kiuchumi na kuwekea vikomo kushiriki katika soko la kazi. Huwa tunaruhusu maudhui yanayotoa mwito wa mipaka ya kijinsia ya kijeshi, utekelezaji wa sheria na kazi za ufundishaji. Pia tunaruhusu maudhui hayo kulingana na mwelekeo wa ngono, wakati maudhui yanatokana na imani za kidini.
    • Utengwaji kijamii, inayomaanisha vitu kama vile kunyima ufikiaji wa nafasi (halisi na za mtandaoni) na huduma za kijamii, isipokuwa kwa utengwaji wa kingono au kijinsia kwenye nafasi ambazo kwa kawaida huwa na mipaka ya kingono au jinsia, kama vile vyoo, spoti na ligi za spoti, afya na vikundi vya usaidizi na shule mahususi.
  • Matusi, ikiwa ni pamoja na yanayohusu:
    • Sifa, ikiwa ni pamoja lakini si tu tuhuma za woga, kutokuwa mkweli, uhalifu wa kawaida na matendo ya kupenda ngono au hali nyingine za ukosefu wa maadili ya kingono.
    • Sifa za kiakili, ikiwa ni pamoja na lakini si tu tuhuma za upumbavu, uwezo wa akili na ugonjwa wa akili pamoja na ulinganishaji usiofaa kati ya makundi ya PC kwa msingi wa uwezo wa akili. Haturuhusu tuhuma za ugonjwa wa akili au matatizo ya kiakili ikiwa ni kwa msingi wa jinsia au mwelekeo wa ngono, kutokana na mjadala wa kisiasa na kidini kuhusu hali ya watu kubadilisha jinsia zao na wanaoingia katika ndoa za jinsia moja na matumizi ya kawaida yasiyo mabaya ya maneno kama vile “ajabu.”
    • Maeneo mengine, ikiwa ni pamoja na, lakini si tu tuhuma za kukosa thamani, kutokuwa muhimu, kuwa na mwonekano mbaya, uchafu.
  • Kauli zinazopendekeza kwamba kilengwa kinasababisha ugonjwa, ikiwa ni pamoja na lakini si tu: “kunifanya kutapika.”
  • Kulaani iliyokusudiwa, isipokuwa kulaani katika muktadha fulani wa kijinsia wakati wa utengano wa watu wanaopendana, ambayo inafafanuliwa kama:
    • Matumizi yanayolengwa ya neno “fanya ngono” au vibadala vya neno “fanya ngono” kwa nia ya kutusi, kama vile “Fanya ngono na [Sifa Iliyolindwa]!”
    • Maneno au kauli za mwito wa kujihusisha katika shughuli ya ngono au mgusano na sehemu nyeti, mkundu, kinyesi au mkojo, ikiwa ni pamoja lakini si tu: nyonya dhakari yangu, busu mkundu wangu, kula uchafu.
Kwa Viwango vya Jumuiya vifuatavyo, tunahitaji maelezo ya ziada na/au muktadha ili kutekeleza:
Usichapishe:
  • Maudhui yanayotoa kwa uwazi bidhaa au huduma ambazo zinalenga kubadilisha mwelekeo wa ngono au utambulisho wa jinsia wa watu.
  • Dhana za kushambulia maudhui, taasisi, maoni, mazoea, au imani zinazohusiana na sifa zilizolindwa, ambazo zinaweza kuchangia madhara ya mwili yanayoweza kutokea, vitisho au ubaguzi dhidi ya watu wanaohusishwa na tabia hiyo iliyolindwa. Meta huangalia ishara anuwai kuamua ikiwa kuna tishio la madhara katika maudhui. Hizi zinajumuisha lakini si tu kwa: maudhui ambayo yanaweza kuchochea vurugu au vitisho vya karibu; ikiwa kuna kipindi cha mvutano ulioongezeka kama uchaguzi au mzozo unaoendelea; na ikiwa kuna historia ya hivi karibuni ya vurugu dhidi ya kikundi lengwa kilicholindwa. Katika visa vingine, tunaweza pia kuzingatia ikiwa mzungumzaji ni mtu maarufu au yuko katika nafasi ya mamlaka.
Katika kesi fulani, tutaruhusu maudhui ambayo vinginevyo yanaweza kukiuka Viwango vya Jumuiya inapobainika kwamba maudhui hayo ni ya tashtiti. Maudhui yataruhusiwa tu ikiwa vipengee vinavyokiuka vya maudhui hayo vimefanywa kama vya tashtiti au kuhusishwa na kitu au mtu ili kumdhihaki au kumsuta.
Kumbuka: ikiwa wewe ni mtumiaji aliye katika Umoja wa Ulaya na unaona maudhui unayoamini yanakiuka sheria za nchi uliko, unaweza kuwasilisha ombi halali la kuondoa maudhui kwa Facebook au Instagram.
Hali ya matumizi ya mtumiaji
Tazama mifano kadhaa ya jinsi utekelezaji unavyoonekana kwa watu kwenye Facebook, kama vile: inavyoonekana kuripoti kitu ambacho unafikiri hakipaswi kuwa kwenye Facebook, kuambiwa kuwa umekiuka Viwango vyetu vya Jumuiya na kuona skrini ya onyo juu ya maudhui fulani.
Dokezo: Tunaendelea kuboresha, kwa hivyo kile unachokiona hapa kinaweza kupitwa na wakati kiasi ikilinganishwa na kile tunachotumia sasa.
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Kuripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Mawasiliano ya baada ya ripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Hali ya kuondoa
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Skrini za onyo
Data
Tazama Ripoti ya sasa ya Utekelezwaji wa Viwango vya Jumuiya
Utekelezaji
Tuna sera sawa ulimwenguni kote, kwa ajili ya kila mtu kwenye Facebook.
Timu za ukaguzi
Timu yetu ya kimataifa ya wakaguzi zaidi ya 15,000 hufanya kazi kila siku kuweka watu kwenye Facebook kuwa salama.
Ushiriki wa mshikadau
Wataalamu wa nje, wasomi, mashirika yasiyo ya faida na watungaji sera husaidia kuweka Viwango vya Jumuiya ya Facebook.
Pata msaada kwa tabia yenye chuki
Jifunze unachoweza kufanya ukiona kitu kwenye Facebook ambacho kinakiuka Viwango vyetu vya Jumuiya.
Tembelea Kituo chetu cha Usaidizi