Dhuluma na Unyanyasaji

Maelezo ya sera

BADILISHA KUMBUKUMBU
Utaratibu wa Sera
Dhuluma na unyanyasaji hufanyika mahali kwingi na huja kwa namna tofauti kuanzia kutoa vitisho hadi kufichua maelezo yanayomtambulisha mtu, kutuma ujumbe wa vitisho na kufanya mawasiliano yasiyotakikana ya ulaghai. Haturuhusu tabia ya aina hii kwa sababu huzuia watu kuhisi kuwa salama na kuheshimiwa kwenye Facebook, Instagram na Threads.
Tunatofautisha kati ya watu maarufu na watu binafsi kwa sababu tunataka kuruhusu mjadala ambao mara nyingi hujumuisha utoaji maoni na watu ambao huchangia katika taarifa za habari au ambao wana hadhira kubwa ya umma. Kwa watu maarufu, tunaondoa mashambulizi ambayo ni ya madhara makubwa pamoja na mashambulizi fulani ambapo mtu huyo maarufu ametambulishwa moja kwa moja katika chapisho au maoni. Tunafafanua watu maarufu kama maafisa wa serikali katika kiwango cha serikali na kitaifa, wagombeaji wa kisiasa wa ofisi hizo, watu walio na zaidi ya mashabiki au wafuasi milioni moja kwenye mitandao ya kijamii na watu wanaopokea habari nyingi.
Kwa watu binafsi, ulinzi wetu huendelea zaidi: Tunaondoa maudhui yaliyokusudiwa kushusha hadhi au kumtia mtu aibu, pamoja na, kwa mfano, madai kuhusu shughuli za ngono za mtu. Tunatambua kwamba dhuluma na unyanyasaji unaweza kuwa na athari ya kihisia haswa kwa watoto, hii ndiyo sababu sera zetu zinatoa ulinzi wa hali ya juu kwa mtu yeyote aliye chini ya umri wa miaka 18, bila kujali hali ya mtumiaji.
Muktadha na nia ni muhimu, na tunawaruhusu watu kuchapisha na kushiriki ikiwa ni bayana kwamba kitu kilishirikiwa ili kukemea na kuvuta nadhari kwenye hali ya dhuluma na unyanyasaji. Katika matukio fulani, tunahitaji mtu kuripoti mwenyewe kwa sababu hiyo hutusaidia kuelewa kwamba mlengwa anahisi kudhulumiwa au kunyanyaswa. Pamoja na kuripoti tabia na maudhui kama hayo, tunahimiza watu kutumia zana zilizopo kwenye majukwaa yetu ili kusaidia kulinda dhidi yake.
Pia tuna Kitovu cha Kuzuia Dhuluma, ambacho ni rasilimali kwa mabarobaro, wazazi na walimu wanaotafuta usaidizi kwa masuala yanayohusiana na dhuluma na mizozo mingine. Kinatoa mwongozo wa hatua baada ya hatua, ikiwa pamoja na maelezo kuhusu jinsi ya kuanzisha mazungumzo muhimu kuhusu dhuluma. Jifunze zaidi kuhusu kile tunachofanya ili kulinda watu dhidi ya dhuluma na unyanyasaji hapa.
Dokezo: Sera hii haiwahusu watu ambao ni sehemu ya mashirika yaliyobainishwa chini ya Sera ya Watu Binafsi na Mashirika Hatari au watu waliokufa kabla ya 1900.
Ngazi ya 1: Ulinzi wa jumla kwa kila mtu:
  • Kila mtu amelindwa dhidi ya:
    • Kuguswa kwa:
      • Kurudia, AU
      • Kunyanyaswa kingono, AU
      • Kuelekezwa kwa idadi kubwa ya watu bila kuombwa mapema.
    • Wito wa kujijeruhi au kujitoa uhai kwa mtu fulani, au kikundi cha watu binafsi.
    • Mashambulio kutokana na hali walizopitia za unyanyasaji wa kingono, dhuluma ya kingono, mateso ya kingono, au dhuluma ya nyumbani.
    • Kauli zenye nia ya kutaka kuhusika katika shughuli ya ngono au kutetea kutaka kuhusika katika shughuli ya ngono.
    • Maoni mabaya ya kingono.
    • Picha au michoro michafu yenye taswira ya kingono
    • Mashambulizi kwa kutumia matamshi machafu yanayohusiana na shughuli za kingono (kwa mfano: kahaba, hawara).
    • Madai kuwa mkasa wa vurugu haukutokea.
    • Madai kuwa watu binafsi wanadanganya kuhusu kuwa mwathiriwa wa mkasa wa vurugu au shambulio la kigaidi, ikiwemo madai kwamba:
      • Wanatenda/kujifanya kuwa mwathirika wa tukio fulani; au
      • Wamelipwa au kuajiriwa ili kuwapotosha watu kuhusu jukumu lao katika tukio hilo.
  • Matishio ya kutoa nambari ya kibinafsi ya simu, anwani ya makazi, anwani ya barua pepe au rekodi za matibabu (kama inavyofafanuliwa katika sera ya Ukiukaji wa Faragha).
  • Wito wa, au taarifa za nia ya kujihususisha kwenye, dhuluma na/au unyanyasaji.
  • Maudhui ambayo yanadhalilisha zaidi au kuonyesha karaha kwa watu wanaoonyeshwa wakiwa katika mchakato wa, au baada tu ya, kupata hedhi, kukojoa, kutapika, au kujisaidia haja kubwa.
  • Kila mtu amelindwa dhidi ya yafuatayo, lakini kwa watu wazima maarufu, ni lazima wafichuliwe kimakusudi:
    • Wito wa kifo na taarifa zinazopendelea kuambukizwa au kukuza hali ya kiafya.
    • Sherehe au kudhihaki kifo au hali ya kiafya.
    • Madai kuhusu magonjwa ya zinaa
    • Taarifa ya udhaifu kuhusu mwonekano wa kimwili.
Ngazi ya 2: Ulinzi wa ziada kwa Watoto, Watu Binafsi au Watu Maarufu wa Upeo Wenye Kikomo Kulenga (kwa mfano, watu ambao umaarufu wao una mipaka katika uanaharakati, uanahabari au wanaopata umaarufu kupitia njia za kulazimishwa):
  • Kando na ulinzi wa jumla kwa kila mtu, watoto wote (watu binafsi na watu maarufu), watu wazima binafsi na watu maarufu wa upeo wenye kikomo wanalindwa dhidi ya:
    • Madai kuhusu shughuli za ngono, isipokuwa kwa muktadha wa tuhuma za jinai dhidi ya watu wazima (mguso wa kingono bila ridhaa).
    • Maudhui ambayo yanampa mtu mzima sifa za ngono (unyanyasaji wa kingono wa watoto umezungumziwa katika Sera ya Unyanyasaji wa kingono wa Watoto, Dhuluma na Uchi).
  • Watoto wote (watu binafsi na watu maarufu), watu wazima binafsi na watu maarufu wa upeo wenye kikomo) wanalindwa dhidi ya yafuatayo, lakini kwa watoto maarufu, lazima wafichuliwe kimakusudi kwa:
    • Ulinganishaji usio na utu (kwa njia ya maandishi au ya kuona) kwa au kuhusu:
      • Wanyama na wadudu, wakiwemo viumbe ambao hawafai kwa wanadamu, ambao wanachukuliwa kuwa dhalili.
      • Bakteria, virusi, vijidudu na magonjwa.
      • Vitu visivyo na uhai, vikiwemo takataka, uchafu, kinyesi.
  • Maudhui ambayo yamekarabatiwa ili kuangazia, kuviringa, au vinginevyo kuvuta nadhari kwa njia hasi kwenye sifa fulani za kimaumbile (pua, sikio, na kadhalika).
  • Maudhui ambayo yanawaweka katika viwango kulingana na mwonekano wa kimwili au sifa za wahusika.
  • Maudhui ambayo yanawadhalilisha zaidi watu ambao wanaonyeshwa wakidhulumiwa kimwili (isipokuwa katika muktadha wa mapambano ya michezo).
Ngazi ya 3: Ulinzi wa ziada kwa Watoto Binafsi, Watu Wazima Binafsi, na Watoto Maarufu Bila Kutaka:
  • Kando na ulinzi wote ulioorodheshwa hapa juu, watoto wote binafsi, watu wazima binafsi (ambao lazima wajiripoti), na watoto maarufu bila kutaka wanalindwa dhidi ya:
    • Kitendo lengwa cha kulaani.
    • Madai kuhusu kuhusika kimahaba, mwelekeo wa kingono au utambulisho wa kijinsia.
    • Wito wa hatua, taarifa za nia, taarifa za matamanio au masharti, au taarifa zinazotetea au kuunga mkono kutengwa.
    • Tabia mbaya au madai ya uwezo usiostahili, isipokuwa katika muktadha wa tuhuma za uhalifu na maoni ya kibiashara dhidi ya watu wazima.
    • Maonyesho ya dharau, karaha au maudhui yanayokataa kuwepo kwa mtu binafsi, isipokuwa katika muktadha wa madai ya jinai dhidi ya watu wazima.
  • Wakati watoto binafsi, watu wazima binafsi, na watoto maarufu bila kutaka wanaojiripoti wanalindwa dhidi ya yafuatayo:
    • Unyanyasaji wa sauti ya kwanza
    • Taswira zisizotakikana ambazo zimefanyiwa ukarabati.
    • Kulinganisha na watu maarufu, wa kubuni au wa kibinafsi kwa msingi wa mwonekano wa kimwili.
    • Madai kuhusu utambulisho wa dini
    • Kulinganisha na wanyama au wadudu ambao kitamaduni wanachukuliwa kuwa wajinga au wanyonge {“chui marara”, “simba”).
    • Ufafanuzi wa wastani au chanya wa kimwili.
    • Tabia zisizo mbaya au madai ya uwezo usiostahili.
    • Mashambulizi kupitia matamshi ya matusi yanayohusiana na ukosefu wa shughuli za ngono.
Ngazi ya 4: Ulinzi wa ziada kwa Watoto Binafsi pekee:
  • Watoto hupata ulinzi mkubwa zaidi chini ya sera yetu. Pamoja na ulinzi wote ulioorodheshwa hapa juu, watoto binafsi pia wanalindwa dhidi ya:
    • Tuhuma kuhusu tabia ya uhalifu au haramu.
    • Picha za dhuluma ya kimwili dhidi ya watoto zilizoshirikiwa na muktadha ya kukashifu
    • Matamshi ya matusi yanayohusiana na jinsia ya kike.
Dhuluma na unyanyasaji kupitia kurasa, vikundi, matukio na ujumbe
  • Ulinzi wa Ngazi ya 1 hadi 4 pia hutekelezwa kwenye kurasa, vikundi, matukio na ujumbe.
Kwa Viwango vya Jumuiya vifuatavyo, tunahitaji maelezo ya ziada na/au muktadha ili kutekeleza:
Usiwahi:
  • Kuchapisha maudhui ambayo yanalenga watu binafsi kupitia Kurasa, Vikundi na Matukio yasiyohitajika. Tunaondoa maudhui haya yanaporipotiwa na mlengwa au mwakilishi aliyeidhinishwa wa mlengwa.
  • Kuchapisha maudhui yaliyofafanuliwa hapa juu ambayo yangehitaji mlengwa kuripoti maudhui au pale ambapo maudhui yanaashiria kuwa chapisho linalenga mlengwa moja kwa moja (kwa mfano: mlengwa ametambulishwa kwenye chapisho au maoni). Tutaondoa maudhui haya ikiwa tuna uthibitisho kutoka kwa mlengwa au mwakilishi aliyeidhinishwa wa mlengwa (aliye hai au aliyekufa) kuwa maudhui hayahitajiki.
  • Kuchapisha maudhui yanayotoa mwito au kusema dhamira ya kushiriki tabia ambayo itastahiki kama uonevu na unyanyasaji chini ya sera zetu. Tutaondoa maudhui haya wakati tuna uthibitisho kutoka kwa mlengwa au mwakilishi aliyeidhinishwa wa mlengwa kuwa maudhui hayahitajiki.
  • Kuchapisha maudhui yanayompa mtu maarufu za kingono. Tutaondoa maudhui haya wakati tuna uthibitisho kutoka kwa mlengwa au mwakilishi aliyeidhinishwa wa mlengwa kuwa maudhui hayahitajiki.
  • Anzisha mawasiliano yanayomnyanyasa mpokeaji kingono. Tutaondoa maudhui yoyote yanayoshirikiwa katika muktadha usiotakikana tunapokuwa na uthibitisho kutoka kwa mpokeaji, au mwakilishi aliyeidhinishwa wa mpokeaji kwamba mguso huo hauhitajiki.
  • Ondoa unyanyasaji wa watu ulioelekezwa, wakati:
    • Inalenga, kupitia sehemu yoyote, 'watu walio katika hatari kubwa ya madhara ya nje ya mtandao', hufafanuliwa kama:
      • Watetezi wa haki za binadamu
      • Watoto
      • Waathiriwa wa matukio/misiba ya vurugu
      • Watu wa upinzani wenye mamlaka katika nchi zilizo katika hatari wakati wa uchaguzi
      • Maafisa wa uchaguzi
      • Wapinzani wa serikali ambao wamekuwa wakilengwa kulingana na hali yao ya upinzani
      • Watu wachache wa kikabila na dini ndogo katika maeneo ya mgogoro
      • Mwanachama wa kikundi kilicho katika hatari na kinachotambulika
    • Kulenga mtu yeyote kupitia maeneo ya kibinafsi, kama vile kikasha au wasifu, na:
      • Maudhui yanayokiuka sera za dhuluma na unyanyasaji kwa watu binafsi au,
      • Maudhui yanayopingwa ambayo yanategemea sifa iliyolindwa
  • Lemaza akaunti zinazohusika na unyanyasaji mkubwa kama sehemu ya yoyote
    • Mitandao ya serikali au inayoshirikishwa na serikali inayolenga mtu yeyote kupitia eneo lolote.
    • Mitandao ya ushindani inayolenga mtu yeyote kupitia eneo lolote na:
      • Maudhui yanayokiuka sera za dhuluma na unyanyasaji kwa watu binafsi au,
      • Maudhui ambayo yanawalenga kulingana na sifa iliyolindwa, au,
      • Maudhui au tabia ambayo vinginevyo huonekana kuwa yanapingwa katika muktadha wa ndani
Hali ya matumizi ya mtumiaji
Tazama mifano kadhaa ya jinsi utekelezaji unavyoonekana kwa watu kwenye Facebook, kama vile: inavyoonekana kuripoti kitu ambacho unafikiri hakipaswi kuwa kwenye Facebook, kuambiwa kuwa umekiuka Viwango vyetu vya Jumuiya na kuona skrini ya onyo juu ya maudhui fulani.
Dokezo: Tunaendelea kuboresha, kwa hivyo kile unachokiona hapa kinaweza kupitwa na wakati kiasi ikilinganishwa na kile tunachotumia sasa.
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Kuripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Mawasiliano ya baada ya ripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Hali ya kuondoa
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Skrini za onyo
Data
Tazama Ripoti ya sasa ya Utekelezwaji wa Viwango vya Jumuiya
Utekelezaji
Tuna sera sawa ulimwenguni kote, kwa ajili ya kila mtu kwenye Facebook.
Timu za ukaguzi
Timu yetu ya kimataifa ya wakaguzi zaidi ya 15,000 hufanya kazi kila siku kuweka watu kwenye Facebook kuwa salama.
Ushiriki wa mshikadau
Wataalamu wa nje, wasomi, mashirika yasiyo ya faida na watungaji sera husaidia kuweka Viwango vya Jumuiya ya Facebook.
Pata usaidizi kuhusu dhuluma na unyanyasaji
Jifunze unachoweza kufanya ukiona kitu kwenye Facebook ambacho kinakiuka Viwango vyetu vya Jumuiya.
Tembelea Kituo chetu cha Usaidizi