Uwakilishi wa Utambulisho Halali

Maelezo ya sera

BADILISHA KUMBUKUMBU
Utaratibu wa Sera
Uhalalishaji ni jiwe msingi la jumuiya yetu. Tunaamini kuwa uhalalishaji husaidia kuunda jumuiya ambapo watu wanawajibika kwa kila mmoja, na kwa Meta, katika njia zenye maana. Tunataka kuruhusu njia nyingi ambapo utambulisho unaonyeshwa kwenye jumuiya yetu ya ulimwengu, huku tukizuia uigaji wa mtu mwingine na uwakilishaji mbaya wa utambulisho. Ili kudumisha mazingira salama na wazi ambapo watu wanaweza kuaminiana na kujenga jumuiya, haturuhusu uundaji wa akaunti au wasifu ambao unaundwa au kutumiwa ili kuwahadaa wengine.
Kwenye Facebook, tunahitaji watu wafungue akaunti moja wakitumia jina wanalotumia katika maisha ya kila siku ambalo linawakilisha utambulisho wao halisi. Tumeunda Wasifu wa Ziada ili kusaidia watu kueleza sehemu tofauti za utambulisho wao, kama vile mapendeleo au biashara zao.
Haturuhusu matumizi ya huduma zetu na tutazuia au kulemaza akaunti za Facebook, Instagram na Threads au vitengo vingine vya Facebook (kama vile Kurasa, vikundi) ambazo:
  • Zinamilikiwa na watoto wenye umri wa chini
  • Zinaiga mtu au shirika jingine kwa:
    • Kutumia picha, jina au mfanano wao kwa lengo la kuwadanganya wengine
    • Kuongea kwa sauti ya mtu au shirika jingine ambalo mtumiaji hajaidhinishwa kufanya hivyo (k.m. kwa kuunda Ukurasa au Wasifu)
  • Zinashiriki katika uwakilishi visivyo wa utambulisho ili kupotosha au kuwadanganya wengine, kukwepa utekelezaji au kukiuka Viwango vya Jumuiya. Tunazingatia vigezo kadhaa tunapotathmini uwakilisho unaopotosha wa utambulisho, kama vile:
    • Mabadiliko ya mara kwa mara au makubwa kwa maelezo ya utambulisho, kama vile jina au umri
    • Maelezo ya kupotosha ya wasifu, kama vile maelezo ya wasifu na eneo la wasifu
    • Kutumia taswira ya akiba
  • Zinatumia jina lililo na ukiukaji wa Viwango vya vyetu Jumuiya.
Kwenye Facebook, tutaomba maelezo zaidi kabla ya kuchukua hatua kuanzia kuzizuia kwa muda hadi kulemaza kabisa wasifu au akaunti za Facebook ikiwa:
  • Umetoa tarehe ya uwongo ya kuzaliwa
  • Unatumia jina ambalo si jina halali unalofahamika kwalo katika maisha ya kila siku
  • Umeunda akaunti moja inayowakilisha au inatumika na zaidi ya mtu mmoja
  • Umeunda au kudumisha akaunti nyingi za Facebook
  • Umeunda akaunti inayowakilisha shiriki lisilo binadamu, kama vile biashara, mnyama kipendwa au mhusika wa kubuni
  • Umedumisha wasifu tupu ambao haujatumika kwa muda
Hali ya matumizi ya mtumiaji
Tazama mifano kadhaa ya jinsi utekelezaji unavyoonekana kwa watu kwenye Facebook, kama vile: inavyoonekana kuripoti kitu ambacho unafikiri hakipaswi kuwa kwenye Facebook, kuambiwa kuwa umekiuka Viwango vyetu vya Jumuiya na kuona skrini ya onyo juu ya maudhui fulani.
Dokezo: Tunaendelea kuboresha, kwa hivyo kile unachokiona hapa kinaweza kupitwa na wakati kiasi ikilinganishwa na kile tunachotumia sasa.
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Kuripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Mawasiliano ya baada ya ripoti
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Hali ya kuondoa
HALI YA MATUMIZI YA MTUMIAJI
Skrini za onyo
Utekelezaji
Tuna sera sawa ulimwenguni kote, kwa ajili ya kila mtu kwenye Facebook.
Timu za ukaguzi
Timu yetu ya kimataifa ya wakaguzi zaidi ya 15,000 hufanya kazi kila siku kuweka watu kwenye Facebook kuwa salama.
Ushiriki wa mshikadau
Wataalamu wa nje, wasomi, mashirika yasiyo ya faida na watungaji sera husaidia kuweka Viwango vya Jumuiya ya Facebook.
Pata usaidizi wa uwakilishi wa utambulisho halali
Jifunze unachoweza kufanya ukiona kitu kwenye Facebook ambacho kinakiuka Viwango vyetu vya Jumuiya.
Tembelea Kituo chetu cha Usaidizi